Kilifi

Mji nchini Kenya


Kilifi ni mji kwenye pwani ya kusini ya Kenya uliopo kati ya Mombasa na Malindi. Iko kando ya kihori cha Kilifi ("Kilifi Creek") kinachoishia katika Bahari Hindi.

Kilifi
Kilifi is located in Kenya
Kilifi
Kilifi

Mahali pa mji wa Kilifi katika Kenya

Majiranukta: 3°38′0″S 39°51′0″E / 3.63333°S 39.85000°E / -3.63333; 39.85000
NchiKenya
KauntiKilifi
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 122,899
Kilifi, Kenya
Madau kwenye kihori cha Kilifi Creek

Mji ni makao makuu ya Kaunti ya Kilifi.

Wakati wa sensa ya mwaka 2009 Kilifi ilikuwa na wakazi 122,899 [1].

Kilifi imekuwa kitovu kimojawapo cha utalii nchini Kenya hasa kutokana na fuko zake za kupendeza na Bofa Beach ni marufuku hasa. Mdomo mpana wa kihori unapendwa na wenye jahazi za burudani, hivyo kuna jahazi nyingi zinazolala hapa.

Historia

hariri

Kulikuwa mahali pa makazi ya Waswahili wa kale.

Maghofu ya kihistoria ya Mnarani yako kando ya mji wa Kilifi. Mabaki yanayoonekana ni misikiti miwili pamoja na makaburi yaliyokuwa sehemu ya mji wa Waswahili uliokuwa kituo cha biashara. Msikiti mkubwa ulianzishwa mnamo mwaka 1425; mji uliangamizwa wakati wa mashambulio ya Waoromo katika karne ya 17.

Tazama pia

hariri

Tanbihi

hariri
  1. Sensa ya Kenya 2009 Archived 9 Januari 2019 at the Wayback Machine., tovuti ya KNBS, ilitazamwa Januari 2009.